Home » » VIDOKEZO MUHIMU KWA WALE WANAOPENDA KUTEMBELEA HIFADHI YA ZIWA MANYARA

VIDOKEZO MUHIMU KWA WALE WANAOPENDA KUTEMBELEA HIFADHI YA ZIWA MANYARA

Hifadhi ya Manyara iko umbali wa kilometa 125 magharibi mwa mji wa Arusha, chini ya ukuta wa bonge la ufa, Hifadhi hii in ukubwa wa kilometa za mraba 330, ambapo kati ya hizo 230 ni Ziwa Manyara.
Hifadhi hii inayo makazi makubwa ya aina nyingi za ndege na wanyama kutokana na ukuta wa bonde la ufa, msitu wa asili ya maji ndani ya ardhi, mapori ya migunga na maeneo ya wazi ya mbuga.
Mnyama wa kuvutia kuliko wote katika hifadhi ya ziwa manyara ni simba wapandao miti, ambao mara nyingine huonekana katika matawi ya migingu.
Wanyama wengine wanaopatikana katika hifadhi ya ziwa manyara ni pamoja na tembo, chui, swala, viboko na mamilioni ya ndege maji (korongo) , ziwa linawavutia ndege wengi kuwepo katika hifadhi ya ziwa manyara.
Hifadhi ya Ziwa Manyara inayo idadi kubwa ya Tembo katika kila kilometa moja.

Huduma kwa wageni;
wapendao kwenda Ziwa Manyara unaobwa kupiga simu +255767492623 na email:info@zlinda.8m.com
www.zlinda.8m.com

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa