Home » » WATAFITI WAOMBWA KUGEUKIA UFUGAJI

WATAFITI WAOMBWA KUGEUKIA UFUGAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WATAALAMU wa utafiti nchini wameombwa kujikita kwenye utafiti wa mifugo na kutoa elimu kwa wafugaji ili waboreshe shughuli zao na kuleta tija kwa kufuga kisasa.
Ombi hilo lilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Elaston Mbwilo wakati wa ufunguzi wa warsha ya mradi wa utafiti wa kilimo kwa kutumia mbolea wa Africa RISING iliyowashirikisha wakulima na wafugaji wa Wilaya ya Babati.
Mbwilo alisema wafugaji wengi nchini hawana maisha bora kwa kuwa mifugo yao haiwasaidii kimaisha katika kujingizia kipato bora kutokana na kutojua mbinu za ufugaji wa kisasa, hivyo hawana budi kuangaliwa kwa upana na kupewa kipaumbele katika masuala ya utafiti.
Alisema idadi ya wakulima na wafugaji katika mkoa huo inalingan, na kwa upande wa wakulima hali zao kimaisha ni nzuri kiasi, huku akibainisha kwamba wamepiga hatua katika kilimo kwa vile wanapata elimu ya mara kwa mara kutoka kwa wataalamu.
Kwa upande wake, mtafiti kilimo wa mradi huo, Festo Ngulo, alitaja maeneo yanayotekelezwa kwenye mradi huo kuwa yanamgusa mfugaji ambayo ni jinsi ya kuzalisha mazao kwa kuongeza kiwango cha mavuno, matumizi ya mbolea yenye virutubisho ya minjingu na malisho.
Mradi huo ulianza kipindi cha mavuno mwaka 2012/13 na utafanyika kwa miaka mitano kwenye wilaya tatu nchini ambazo ni Babati na Kiteto, Manyara na Kongwa mkoani Dodoma kutokana na hali ya hewa na rutuba za maeneo hayo.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa