Home » » MAENEO ZAIDI YA 500 NCHINI HAYAKUSHIRIKI UCHAGUZI

MAENEO ZAIDI YA 500 NCHINI HAYAKUSHIRIKI UCHAGUZI

Licha ya uchaguzi wa viongozi wa ngazi za mitaa, vijiji na vitongoji kakamilika mwezi uliopita, maeneo karibu 500 hayakuchagua viongozi kwa sababu mbalimbali.
Kufuatia madai hayo NIPASHE iliwasiliana na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Khalist Luhanda,kuufahamu ukweli.
Tamisemi ilikiri kuwa ina taarifa za mitaa, vitongoji na vijiji karibu 500 kukosa viongozi wapya.
Alisema maeneo hayo hayana viongozi wapya baada ya wananchi kukataa kuwachagua kwa sababu mbalimbali zikiwamo kuishinikiza serikali kuvipa vitongoji hadhi ya kijiji. Baadhi ya vijiji wananchi walitaka kijiji kigawanywe na wapo waliotaka
maeneo yao yawe kata ilhali maeneo yenyewe hayakidhi vigezo.”
Alisema wasimamizi wa uchaguzi ambao ni Wakurugenzi wa Halmashauri, wameelekezwa kuhakikisha ifikapo mwisho wa mwezi huu maeneo yote yawe yamefanya uchaguzi uliobakizwa viporo.
“Isipokuwa maeneo ambayo hayakufanya uchaguzi kutokana na waliyokuwa wagombea kufariki na yale ambayo wananchi kwa sababu mbalimbali waliteketeza kwa moto, nyaraka na vifaa vyote vya uchaguzi, kwamfano baadhi ya maeneo mkoani Sumbawanga, itachukua muda kidogo uchaguzi kufanyika,” alieleza Luhanga.
Luhanga alisema katika maeneo hayo, serikali italazimika kufanya maadalizi ya uchaguzi upya, ikiwa ni pamoja na kuandika upya majina ya wapiga kura na wagombea.
Kwa mujibu wa maelezo yake, wamebaini kasoro kadhaa zitakazolazimisha uchaguzi huo kurudiwa katika baadhi ya maeneo.
Hadi anatoa taarifa hizo, alisema serikali ilikuwa ikiendelea na jitihada za kuhimiza wananchi hao kutumia fursa itakayotolewa ya kurudia uchaguzi, kuchagua viongozi wao vinginevyo waziri mhusika atatumia mamlaka ya kisheria, kuhakikisha hakuna eneo litakalobaki bila uongozi.
Alibainisha pia kwamba, maeneo yote yaliyokumbwa na sintofahamu wakati wa kuapisha viongozi waliyopatikana kwa njia halali ya uchaguzi, kiasi cha kusababisha wananchi kuapisha waliyodai kuwa ndiyo viongozi wanaowataka pia yatafanya uchaguzi upya
“Kwa mfano wale Wamasai ambao waliapisha kiongozi wao kimila,watabaki naye lakini serikali haitambui uongozi wa aina hiyo, hivyo uchaguzi utarudiwa ili kupata anayetambuliwa kisheria,”alieleza Luhanga.
Alisema maandalizi ya marudio ya uchaguzi huo, yanaendelea na kwamba wakati wowote baada ya mwisho wa mwezi huu watatoa taarifa, ikielekeza kitakachotakiwa kufanyika, ili kuhakikisha kila eneo nchini linapatiwa uongozi wa kiserikali unaoeleweka, kwa mujibu wa sheria.
CHANZO: NIPASHE
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. KUELEKEA UCHAGUZI 2015: JE UNAPENDA NANI AWE KIONGOZI WAKO? JAZA FOMU HII FUPI HAPA docs.google.com docs.google.com

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa