Mgogoro
wa kugombea madaraka ya uwenyekiti wa kijiji cha kambi ya chokaa
wilayani Simanjiro umeingia katika uvunjifu wa amani baada ya mmoja wa
wajumbe wa serikali ya kijiji anayemuunga mkono mgombea aliyependekezwa
na CCM Mbiki Ratoi Bwana Yohana Rometi kuuawa kwa kupigwa na vitu vyenye
ncha kali na wananchi wanaodaiwa kuunga mkono upande wa pili.
ITV ilifika katika kijiji cha kambi ya chokaa katika maziko ya
mjumbe huyo wa serikali ya kijiji ambaye anatajwa kumunga mkono mgombea
mmoja kati ya wanaogombania nafasi hiyo anayedaiwa kuuawa na mashabiki
wa upande wapili katika vurugu zilizofanyika kijjijini hapo na
kushuhudia watu wenye uzuni na machozi baada ya mwili wa marehemu Yohana
Rometi kuwasiri ukitokea hospitali ya KCMC mkoani Kilimanjaro.
Akizungumza na ITV kaka wa marehemu Yohana Rometi Bwana John Rometi
amesema tukio ilo limewatisha na anashindwa kuamini kuwa watanzania
sasa wamefikia hatua ya kutoana uhai kwa ajili ya ushabiki wa kisiasa
tena kwa chama kimoja huku akiiomba serikali itende haki na mmoja wa
viongozi wa serikali ya kijiji hicho Kiberesa Kunei akiwataka familia ya
marehemu kuto lipiza kisasi kwani wameshaikabidhi serikali kuchukua
hatua.
Akihubiri katika ibada ya maziko mchungaji kiongozi wa kanisa la
KKKT usharika wa nomieuti wilaya ya Simanjiro Nurueli Mbaga amesema
watanzania wa leo wamekuwa wabaya kuliko wanyama kwani zuruma uonevu na
ukatili vimeshika nafasi kuliko haki huku mwenyekiti aliyepitishwa na
CCM anayedaiwa kuungwa mkono na marehemu ambaye ameapishwa tarehe 29
mwezi decemba mwaka jana Mbuki Molel Ratoi akiwasii wananchi kuacha
visasi kwakuwa havina nafasi kwa sasa.
Chanzo:ITV Tanzania
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment