Home » » NYALANDU AENDELEA KUTEMA CHECHE MANYARA

NYALANDU AENDELEA KUTEMA CHECHE MANYARA

Naibu waziri wa maliasili na utalii Lazaro Nyalandu amesema, serikali itahakikisha wote waliovamia hifadhi ya taifa ya tarangie wanachukulia hatua za kisheria kwa haraka ili kuinusuru hifadhi hiyo.

Amesema uvamizi huo umechangia kwa kiwango kikubwa kukithiri kwa ujangiri kwa wanyama kama vile tembo na uhaibifu mwingine wa mazingira katika hifadhi hiyo.
Naibu waziri huyo wa maliasili na utalii, ametoa tamko hilo kwenye kikao cha ujirani mwema kati ya  kamati za ulinzi na usalama za mikoa ya dodoma na manyara,zilizoketi,  kutafuta ufumbuzi wa kutatua mgogoro baina ya wavamizi katika pori la mkungunero lililoko  mpaka wa hifadhi ya taifa ya  tarangire na mkoani manyara na dodoma.

Waziri nyalandu amesema,lengo la wizara yake ni kuona hifadhi za taifa zinalindwa kwa kiwango cha juu ili ziwe endelevu.

Mkuu wa Mkoa Wa Dodoma Dk Rehema Nchimbi na Mkuu Wa Mkoa Wa Manyara Elaston Mbwillo wamesma kuwa ili kuumaliza mgogo huo ni lazima mpaka wa eneo hilo lenye mgogoro uhakikiwe upya.

Pia wamesema ni lazima jamii iliyovamiwa eneo la hifadhi hiyo
ielimishwe ili kufahamu umuhimu wa hifadhi za taifa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa