Home » » WAASWA KUONDOKANA NA KILIMO CHA MAZOEA

WAASWA KUONDOKANA NA KILIMO CHA MAZOEA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Wakulima wameaswa kuondokana na kilimo cha mazoea, badala yake watumie kanuni bora za kilimo ili  waweze kuongeza kiwango cha uzalishaji na kipato katika familia zao.
Mtafiti Mkuu wa Kituo cha Utafiti Seliani Arusha (Sari), Steven Lyimo alisema hayo juzi kwenye maadhimisho ya Siku ya Wakulima ya uboreshaji wa jamii ya mikunde kwa mazao mengi katika kilimo mseto cha mahindi na mbaazi yaliyofanyika Kata ya Singe wilayani Babati.
Alisema kutokana na mabadiliko ya tabianchi ya eneo la Babati na Karatu, wakulima wanalazimika kutumia mbegu za muda mfupi na kati ili waweze kupata wigo mpana wa uchaguzi wa mbegu anapotaka kwenda shambani.
“Inatakiwa mwaka ambao hakuna mvua unapanda mbegu ya muda mfupi, mwaka ambao kuna mvua kiasi unapanda mbegu ya muda wa kati na mwaka ambao kuna mvua ya kutosha unapanda ya muda mrefu,” alisema Lyimo
 Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa