Home » » UKAWA jiandaeni kushindwa-CCM

UKAWA jiandaeni kushindwa-CCM

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (UKAWA), Bw. Edward Lowassa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), wajiandae kushindwa katika Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25, mwaka huu.
Kimesema wapambe wa Bw. Lowassa walimdanganya na kumshawishi ahame CCM kwenda CHADEMA akidai waliomshawishi walimpoteza.
Kauli hiyo imetolewa Dar es Salaam jana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa, Bw. Nape Nnauye wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya ushiriki wao katika uchaguzi huo na nafasi ya ushindi.
Alisema CCM kinaamini kuwa, baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kumtangaza mshindi wa nafasi ya urais, viongozi wa UKAWA wajiandae kupelekwa majumbani mwao kwa gari la kubebea wagonjwa.
Aliongeza kuwa, CCM haishindani na wapinzani bali inashindana na makapi akisisitiza kuwa, hao wanaojiita wapinzani wametokea CCM; hivyo Tanzania hakuna mpinzani.
"Yanga ikicheza na Lipuli, kila mtu anajua matokeo yatakuwaje hivi sisitunajua matokeo yetu wazi...tuna nafasi kubwa ya ushindi kwa asilimia zote na tutashinda asubuhi kweupe kabla ya Oktoba 26, mwaka huu," alisema.
Bw. Nnauye alisema; "Augustino Mrema wakati anahama CCM kwenda NCCR-Mageuzi mwaka 1995, aliondoka kwa mwembwe kama hizi ambazo tunaziona, lakini kilichotokea, nadhani kila mtu alikiona," alisema.
Alifafanua kuwa, chama hicho hakifanyi kazi kwa shinikizo la mtu; bali kinazingatia sheria na kanuni za chama zinavyosema akidai anayetaka kuondoka CCM, aondoke ila chama kitaendelea kuwepo.
Akizungumzia majimbo yaliyowekwa kiporo na Halmashauri Kuu yachama hicho, alisema baada ya vikao vyao kumalizika Mjini Dodoma,kazi iliyobaki ni kuyajadili majimbo 11 yaliyokuwa yamebaki.
"Hadi sasa, Kamati Kuu imeyajadili majimbo tisa na bado inaendelea na vikao ili kuyamaliza yote...majimbo yanayoendelea kujadiliwa ni Singida Mashariki na Kiteto, mkoani Manyara," alisema.
Aliwataja walioshinda katika majimbo tisa kuwa ni Jerry Silaa (Ukonga),Edward Mwalongo (Njombe Kusini), Venance Mwamoto (Kilolo), Raphael Chegeni (Busega), Edwin Ngonyani (Namtumbo), Mohamed Mchengerwa(Rufiji), Norman Sigalla (Makete), Martin Msuha (Mbinga Vijijini) na Joel Mwaka (Chilonwa).

CHANZO MAJIRA


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa