Home » » Daktari mwizi chupuchupu kwenda jela

Daktari mwizi chupuchupu kwenda jela

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

DAKTARI wa Hospitali ya Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, Dk Godson Kato amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini ya Sh 200,000 baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la matumizi mabaya ya nyaraka na kujipatia Sh 800,000 za mwajiri wake.

Dk Kato alisomewa hukumu hiyo juzi ya kwenye mashtaka ya matumizi mabaya ya fedha za umma na Hakimu wa Mahakama ya wilaya hiyo Majid Hudi, ambapo alilipa faini hiyo Sh 200,000 na kuachiwa huru.

Hata hivyo, mshtakiwa wa pili wa kesi hiyo namba 409/2012, Charles Simon ambaye ni Mhasibu Msaidizi wa Halmashauri ya wilaya hiyo aliyeidhinisha Dk Kato kupatiwa fedha hizo, aliachiwa huru baada ya kuonekana hana hatia.

Awali, mwendesha mashtaka wa kesi hiyo Isidore Kyando wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) mkoani Manyara, alisema kuwa Dk Kato alitenda kosa hilo Novemba 20 mwaka 2012.
Kyando alisema Dk Kato aliomba kwa mwajiri wake ambaye ni Halmashauri ya wilaya ya Kiteto fedha hizo Sh 800,000 kwa ajili ya kwenda katika semina hewa vijijini na mhasibu huyo Simon akashirikiana na mhalifu kumwidhinishia fedha hizo.

Alisema mganga huyo aliandaa semina hewa huko vijijini na kuomba kiasi hicho cha fedha Sh 800,000 kwa jili ya kutoa elimu kwa wananchi na akapatiwa fedha hizo, ila hakutimiza hilo aliloliombea ambapo alijinufaisha yeye mwenyewe.

Akitoa hukumu hiyo Hakimu Hudi alimhukumu Dk Kato kwenda jela kwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja au kulipa faini ya Sh 200,000 kwa kosa hilo ambapo alizilipa na mshtakiwa wa pili Mhasibu Simon aliachiwa huru.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa