Home » » NBM YAFUNGUA TAWI LAKE JIPYA MJI MDOGO WA HAYDOM MKOANI MANYARA

NBM YAFUNGUA TAWI LAKE JIPYA MJI MDOGO WA HAYDOM MKOANI MANYARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Sara Msafiri Ally ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Hanang (wa tatu kulia) kikata utepe kuashiria uzindua wa jengo la tawi la NMB lililopo katika mji mdogo wa Haydom. Wa pili kulia ni Meneja wa NMB Kanda ya Kati, Straton Chilongola.
 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Sara Msafiri Ally ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Hanang akizindua jengo la tawi la NMB lililopo katika mji mdogo wa Haydom.

KILIO cha wakazi wa jimbo la Haydom wilaya ya Mbulu mkoani Manyara cha kukosa huduma za kibenki toka Tanzania ipate uhuru,kimepata ufumbuzi wa kudumu baada ya NMB benki, kufungua tawi katika mji mdogo wa Haydom. 
Kwa mujibu wa mbunge wa jimbo la Haydom, Flatei Massay, katika kipindi chote hicho, wananchi wa jimbo hilo wamekuwa wakilazimika kufuata huduma za kibenki Mbulu mjini, umbali wa zaidi ya kilometa 90.  

Mbunge Massy alisema kitendo cha kufuata huduma za kibenki umbali mrefu kiasi hicho, kumekuwa na madhara mengi na makubwa, ikiwemo gharama kubwa ya usafiri na pia usalama wa fedha. “Umbali huo umesababisha wakulima, wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla, kutunza fedha zao majumbani. 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa