Home » » TANZANITEONE YATOA MSAADA WA KISIMA

TANZANITEONE YATOA MSAADA WA KISIMA



na Efracia Massawe, Simanjiro
WANAKIJIJI wa eneo la Naisinyai wilayani Simanjiro mkoani Manyara wameondokana na adha ya tatizo la maji lililokuwa likiwakabili kwa muda mrefu, baada ya Kampuni ya TanzaniteOne kujenga kisima cha kusafisha maji katika eneo hilo.
Akizungumza na Tanzania Daima kutoka Manyara jana Ofisa uhusiano wa Kampuni hiyo, Dotto Medard alisema kuwa kampuni hiyo imechukua jukumu la kujenga na kukabidhi kisima hicho kwa kituo cha Polisi ‘post’ kwa ajili ya matumizi ya kijiji.
Aidha, alitanabanaisha kuwa kisima hicho kimegharimu sh milioni 60 na kitakuwa msaada katika wilaya hiyo hususan katika kusafisha maji yanayotoka katika mabomba mbalimbali kwani kijiografia eneo hilo lina maji chumvi ambayo nayo si salama kwa matumizi.
“Kushirikiana na kijiji si mara yetu ya kwanza, hata hivyo mara nyingi tunashirikiana na viongozi husika kabla hatujafanya jambo lolote, hivyo kisima hiki kitatumiwa na wanakijiji wa ndani na nje ya eneo hili,” alifafanua Medard.
Naye Mkuu wa mkoa huo, Erasto Mbwilo, alitabanaisha kuwa msaada wa kampuni hiyo umekuja wakati muafaka kwa sababu mbali na wanakijiji hao kutumia maji chumvi, lakini bado serikali haikubaliani ni lini ingetatua tatizo hilo.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa