Home » » Manyara watenga bajeti ya mabilioni ya fedha

Manyara watenga bajeti ya mabilioni ya fedha

Mkoa wa Manyara kwa mwaka umekadiria kutumia Sh165.3 bilioni kwa ajili ya kutengeneza bajeti yake ya miaka ya 2014/15 na 2016/17.
Katibu Tawala Msaidizi (Mipango na Uratibu) Samwel Tenga, alisema Sh128.23 bilioni katika fedha hizo, ni za matumizi ya kawaida.
Tenga alisema kiasi kinginge cha Sh37.07, bilioni ni kwa ajili ya kugharimia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Katibu huyo alisema Sh10.58 bilioni katika fedha za matumizi ya kawaida, zitatokana na vyanzo vya mapato vya ndani vya mamlaka za serikali za mitaa.
Alisema ingawa bajeti inayoidhinishwa inashuka kila mwaka, lakini kuna changamoto kadhaa zilizojitokeza katika uidhinishaji wa bajeti hiyo.
Alisema katika kipindi cha miaka mitatu (3) iliyopita ofisi ya mkuu wa mkoa iliidhinisha Sh8.228 za maendeleo lakini zilitolewa Sh5.058, bilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa