Home » » Mazao mbalimbali kuvunwa karibuni

Mazao mbalimbali kuvunwa karibuni

 JUMLA ya tani 450,330 za mazao ya chakula na tani 51,930 za mazao ya biashara ya wakulima zinatarajiwa kuvunwa wilayani Simanjiro, mkoani Manyara, baada ya kulima hekta 148,935 za mazao ya biashara na hekta 51,930 za mazao ya chakula.
Akisoma taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Elaston Mbwilo, Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Elias Ntiruhungwa, aliyasema hayo jana wakati akisoma taarifa ya wilaya ya Simanjiro kwa mkuu wa mkoa huo Elaston Mbwilo, kwenye ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo.
Ntiruhungwa alisema hadi mwishoni mwa Desemba mwaka jana wilaya hiyo ilikuwa imepata wastani wa mvua milimita 58 ambayo ni kidogo kwa shughuli za kuandaa mashamba na kusababisha wakulima wengi kushindwa kuyatayarisha.
Hata hivyo, alisema wilaya hiyo imekwisha sambaza vocha za pembejeo za ruzuku kwa wakulima wa vijijini katika utekelezaji wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) wilayani humo.
Kwa upande wake, mkuu wa mk o a h u o , Mbwi l o aliwataka viongozi wa wilaya hiyo kuwahesabu wafugaji ili kuondoa dhana ya wakazi wa Simanjiro wanakabiliwa na njaa kwani wengi wao wanauwezo wa kununua chakula.
"Siamini kama Simanjiro wana njaa kwani wana ng'ombe wengi na ng'ombe mmoja anauzwa hadi sh.500,000 hivyo watumie mifugo yao ili iwasaidie na siyo kudai kwamba wana njaa ya chakula," alisema Mbwilo.
Alisema wafugaji wengi hawajapewa elimu ya kutosha juu ya ufugaji wenye tija ndiyo sababu wanakuwa na mifugo mingi isiyokuwa na faida kwao, kwani wana uwezo wa kununua chakula na siyo kulalamikia njaa.

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa