Home » » DC AOMBWA KUINGILIA KATI MGOMO WA WANANCHI

DC AOMBWA KUINGILIA KATI MGOMO WA WANANCHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MKUU wa Wilaya (DC) ya Hanang’, Christine Mndeme, ameombwa kuingilia kati suala la wananchi wa Kata ya Endasak kugoma kuchangia ujenzi wa maabara katika shule ya sekondari ya kata yao.
Akichangia mada kuhusu elimu katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo, Diwani wa Viti Maalumu, Dainesi Hosea (CCM), alieleza wananchi wamekuwa kikwazo katika kuendeleza ujenzi huo kwa kukataa kuchangia wakidai hawaoni faida ya ujenzi huo.
Mkuu huyo wa wilaya, alibainisha suala la wananchi kuchangia elimu halina ubishi na kumtaka diwani huyo kuwahamasisha na kuwapa elimu ya kutosha wananchi wake kuchangia ujenzi huo kabla ya ofisi ya mkurugenzi haijafika katika eneo lake.
“Ile nguvu tuliyoonyesha wakati wa kuchangia ujenzi wa shule za kata na tuzitumie katika kujenga maabara katika shule hizo, hivyo basi wewe diwani uende ukawahamasishe wananchi wako wachangie kabla mkurugenzi hajafika kuhamasisha wananchi hao,” alisisitiza mkuu huyo wa wilaya.
Hata hivyo, Mndeme alisema suala la Shule ya Sekondari Sirop ni la kusikitisha hasa kwa kuwa na elimu duni inayochangia shule hiyo kufeli kila mwaka na kuahidi kuifanyia mabadiliko kwa kushirikiana na wananchi na madiwani wa wilaya hiyo.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa