Home » » MISS REDD's MANYARA 2014 KUPATIKANA JUMAMOSI HII

MISS REDD's MANYARA 2014 KUPATIKANA JUMAMOSI HII

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na Bertha Mollel -Manyara

Warembo wapatao  14 kutoka vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Manyara wameingia kambini mapema jana kwa lengo la kujifua kwa maandalizi ya kinyang’anyiro cha kumsaka mlimbwende wa mkoa huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 14 katika ukumbi wa CCM hall iliyoko wilayani Babati.

Akizungumza na Tanzania daima, mratibu wa mashindano hayo Akon Clement kupitia kampuni ya mererani Entartainment aliwataja warembo walioingia kambini  kuwa ni Happy Wilium, Edna Mushi, Merry Ruta, Rose Evason, Flora Godlizen, Amina Omary, Catherine  Emmanuel, Sabrina Anger, Bertha Fredrick na Samila.

Alisema kuwa warembo hao ni kutoka katika vitongoji vya babati,  simanjiro na mbulu ambao wameingia rasmi kambini   mapema ili kuweza kupatiwa elimu na mazoezi   juu ya kinyang’anyiro hicho hasa hasa ikiwemo kuwajengea  uwezo wa kujiamini na kujithamini.

Alisema kuwa shindano hilo la kumsaka malkia wa Mkoa wa Manyara litasindikizwa na burudani  kutoka kwa wasanii mbalimbali wa mkoa wa Manyara na msanii maalumu kutoka jijini Dar- es-  salaam Bob Junior akipiga hatua kwa hatua kushusha nyimbo  zake mbalimbali zilizobamba kwenye vyomba vya habari.

Akon alisema kuwa  Shindano hilo la aina yake mjini Babati limedhaminiwa na makampuni mbalimbalia wakiwemo kampuni ya TBL kupitia kinywaji chake cha Redd’s original,  Kifaru  Agrovet, Winners Hotel,  wadhamini wengine ni Active classic Fashion, Open University, kimweri sport wear, Manyara Computer  pamoja na Sarafina Lodge.

“Mimi niseme tu kuwa kwa maandalizi tuliyoyafanya na burudani mbalimbali tulizoziandaa, niwatonye tu mashabiki na wadau wa urembo na burudani wa mkoa wa Manyara kuwa watafurahi na kuburudika vya kutosha na hivyo waj itokeze  kwa wingi bila kukosa katika kinyang’anyiro hicho

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa