Home » » UKOSEFU WA VYAMA VYA MICHEZO NI SABABU YA KUZOROTA KWA MICHEZO MKOANI MANYARA

UKOSEFU WA VYAMA VYA MICHEZO NI SABABU YA KUZOROTA KWA MICHEZO MKOANI MANYARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na Betha Mollel
Ukosefu wa umoja au vyama vya michezo wilayani Hanang' iliyoko mkoani Manyara, imeelezwa kama chanzo cha kudorora kwa michezo mingi katika wilaya hiyo ingawa washabiki wapo wa kutosha na wenye vipaji kadhalika.
Akizungumza na Tanzania daima, Ofisa Utamaduni wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang’ James Surumo alisema kuwa wilaya hiyo haina vyama vya michezo mingi, ila chama cha soka wilaya ya Hanang’ (HDFA) ndicho kipo hai na viongozi wake wa wilaya ambao wanasimamia kandanda pekee hali ambayo michezo mingine inakosa nafasi kutokana na kukosa hamasa.

Alisema kuwa wakati Serikali inaandaa sera ya michezo ingepaswa iende sambamba na  vyama vya michezo husika vinavyopaswa kuzisimamia, endapo  Hanang' kungekuwa na viongozi wa vyama hivyo vya michezo wilayani humo, wanamichezo wangepiga hatua na kupatia sifa wilaya hiyo.

Alisema kwenye wilaya hiyo, vijana wengi wanapenda kucheza michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa wavu, pete, kikapu, riadha na mingineno ila kutokana na ukosefu wa viongozi wa vyama hivyo vipaji hivyo hufa.

“Vipaji vingi vinashindwa kuendelezwa kutokana na kutosimamiwa ipasavyo hivyo hufa kabla ya kutumika ila viongozi hao wangekuwa na vyama hivyo Hanang’ tungepiga hatua kubwa kwenye michezo,” alisema Surumo.

Miaka iliyopita wilaya ya Hanang’ ilibahatika kuwa na wanariadha wengi mahiri, akiwemo mwanariadha wa kimataifa, Gidamis Shahanga ila hivi sasa vipaji vipya vimeshindwa kuibuliwa na kutowepo kwa wanaridha wapya.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa