Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wakulima hao walipatiwa elimu hiyo na maofisa
ugani kazi 10, ambao kati yao watano walikuwa Kijiji cha Kakoi na
wengine watano kwenye Kijiji cha Endadosh.
Hayo yalielezwa na ofisa mazao wa mradi wa
uzalishaji na masoko wa shirika la Farm Africa, Tumaini Elibariki wakati
akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Mkulima iliyofanyika jana
kwenye kijiji cha Endadosh, Kata ya Qash.
Elibariki alisema kwa kutumia vifaa hivyo,
wakulima wengi wamenufaika navyo kwa kuwa sasa wanafuata kanuni bora za
kilimo cha ufuta, ikiwemo kuandaa mashamba, mbegu bora na mbinu za
kilimo bora kwa njia rahisi kuliko kuwatumia maofisa ugani.
“Lengo letu ni kila mkulima mwenye kifaa hicho,
azifikie kaya za wakulima 50 kwa muda wa miezi sita, ili wanufaike na
kilimo hicho na kutekeleza kauli mbiu ya “ufuta mafuta, mafuta hufuta
jasho”,” alisema Elibariki.
Alisema kwa kutumia kilimo cha ufuta, wakulima wa
Tarafa ya Mbugwe wilayani humo, wameweza kunufaika kiuchumi kwa kuwa
awali wengi wao walikuwa na nyumba za tembe, lakini sasa wamejenga
nyumba bora za kisasa.
Naye ofisa kilimo wa Mkoa wa Manyara, Coletha
Shayo aliwataka wakulima kulima zao hilo kwa kuwa lina faida kubwa.
Alisema ekari moja inaweza kutoa magunia sita yenye thamani ya Sh1.8
milioni.
“Katika kilimo chenye faida kwa mkulima kwa sasa
ni kilimo cha ufuta kwani unaweza kutumia gharama za Sh200,000 hadi
Sh300,000 kuandaa shamba, mbegu, kupanda, kupalilia na kuvuna na ukapata
Sh1.8 milioni,” alisema Shayo.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment