Home » » Akatwa kichwa mapigano ya wakulima, wafugaji

Akatwa kichwa mapigano ya wakulima, wafugaji

Kiteto. Mapigano baina ya wakulima na wafugaji wilayani Kiteto Mkoa wa Manyara yameibuka tena na kusababisha mtu mmoja kuuawa kwa kukatwa kichwa katika Kijiji cha Kondevesi.
Tukio hilo ni la pili ndani ya wiki moja, ambapo awali watu wawili waliuawa na wengine nane kujeruhiwa katika ugomvi wa aina hiyo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Akili Mpwapwa alithibitisha kuuawa mfugaji huyo.
“Ni kweli kuna mfugaji wa kimasai ameua, jina lake halijatambuliwa na msako wa kuwakamata waliohusika umeanza,” alisema Mpwapwa. “Ni mapigano ya kulipiza kisasi baada ya awali wakulima kuwashambulia wafugaji wakulima na kuamua na kujeruhi,” aliongeza Mpwapwa.
Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kiteto, Dk Thomas Ndalio alisema hali za majeruhi saba kati ya wanane waliolazwa katika hospitali hiyo zinaendea vizuri.
DK Ndalio alisema majeruhi mmoja, Musa Juma hali yake ni mbaya na aliwahishwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Aliwataja majeruhi waliokatwa kwa sime, mikuki na visu kuwa ni mtoto wa miaka 12, Juma Bahati, Emmanuel Mathias (26), Hoti Damiani (38), Mwajuma Hamis (20).
Wengine ni Habiba Ally (16) na Mwajuma Martin (33) ambao wote bado wanapewa matibabu.
Dk Ndalio alisema katika mapigano hayo yaliyotokea Desemba 21 mwaka, huu alipokea miili ya watu wawili waliouawa katika eneo la mapigano Kijiji cha Olpopong wilayani humo.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa