Home » » Wawili wakamatwa na mirungi Manyara

Wawili wakamatwa na mirungi Manyara

JESHI la Polisi mkoani Manyara linaendelea na msako katika wilaya zake, hasa maeneo ya vijijini kwa lengo la kudhibiti na kukomesha uhalifu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuku za mwisho wa mwaka.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Mussa Marambo, alisema jana kuwa katika msako uliofanyika katika vijiji vya Olasiti na Vilima kwa siku tano, walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili waliodaiwa kukutwa na mirungi na mtuhumiwa mwingine alitoroka.
Alisema mtuhumiwa Tumaini Mrema alikamatwa katika Kitongoji cha Mdori akiwa na kilogramu tano za mirungi ndani ya basi la Ntoku lenye namba T 342 BXN, lililokuwa likitokea Arusha kuelekea Singida.
Marambo alisema mtuhumiwa mwingine, Mussa Kamari ambaye ni dereva wa basi la Kampuni ya Mohamed Classic lenye namba T 163 AJR linalofanya safari zake Arusha na Mwanza, alikamatwa na kilogramu 10 za mirungi katika Kijiji cha Olasiti.
Alimtaja mtuhumiwa aliyetoroka kuwa ni Sawa Maliki, mkazi wa Kijiji cha Vilima Vitatu na kusema kuwa alikutwa na pombe aina ya gongo lita 40 pamoja na mtambo wa kutengenezea pombe hiyo. Polisi wanaendelea kumsaka
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa