Manyara.Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Eraston Mbwilo, amewataka
wafanyakazi mkoani humo kufanya kazi kwa uadilifu na kufuata sheria kwa
kutoa huduma stahiki kwa wateja wao, ili kuboresha ufanisi wa kazi zao.
Wito huo ameutoa jana wakati wa baraza la kwanza
la wafanyakazi la mwaka 2014 la mkoa huo, ambapo alisema wafanyakazi
huongozwa na sheria hivyo hawana budi kuzifuata.
Awali akifungua baraza hilo, Mbwilo alisema,
wafanyakazi wengi hawazingatii sheria na uwajibikaji katika kazi zao
hususani suala la muda, kwani wapo watu waliojenga mazoea ya kuchelewa
kuingia na kuwahi kutoka kazini.
“Wafanyakazi tunahitajika kuzingatia muda wa
kuingia ofisini kwa kuwa sheria zinatubana lakini tunawaonea sana
wahudumu wa ofisi, hawa ndiyo sheria zinawabana zaidi maana wanawahi
kuingia kazini, utakuta saa 1.30 muhudumu tayari anafanya usafi,”
alisema Mbwilo. Alilitaka baraza hilo kujadili suala la uadilifu kwa
wafanyakazi ikiwa ni pamoja na matumizi ya lugha nzuri na zenye
kuridhisha za kuwaweka karibu zaidi na wateja pindi wanapofuata huduma
kwenye ofisi zao.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment