Babati. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa
wa Manyara, imewataka wafanyabiashara kuendelea kutumia mashine za
kielektroniki (EFD) ili kuwarahisishia utunzaji kumbukumbu na ukadiriaji
kodi.
Akizungumza kwenye jukwaa la wadau juzi, Ofisa
Kodi Msaidizi wa TRA mkoani Manyara, Fredy Peter alisema mashine hizo
zina uwezo wa kutunza kumbukumbu za mauzo, ununuzi na mali za biashara
bila kufutika kwa muda usiopungua miaka mitano na kuondoa usumbufu wa
kuchapisha vitabu vya risiti.
“Sheria inamtaka mfanyabiashara anyeuza au kutoa
huduma ya sh5000 na zaidi atoe risisti na pia atalazimika kuchapisha
vitabu vya risiti mara zote na sasa zinatumika mashine ili kuondokana na
uchapishaji wa vitabu,” alisema.
Alisema mfumo huo ni wa awamu ya pili kutekelezwa
na unawalenga wafanyabiashara ambao hawajasajiliwa kwenye uongezeko la
thamani (VAT) ambao mauzo ghafi yao kwa mwaka ni sh14 milioni na zaidi.
Aliwataja walengwa wa awamu hiyo kuwa ni wenye
maduka ya jumla, ya vipuri, mawakili, wafanyabiashara wa mbao na
migahawa mikubwa, maduka ya simu, baa na vinjwaji baridi, studio za
picha, wauzaji wa pikipiki na maduka makubwa ya nguo.
Nao, wadau hao waliutaka uongozi wa TRA kufuatilia
makampuni matatu ya usambazaji wa mashine hizo ambayo ni Maxocom
Africa, Webtechnologies na Power Computers ili kuhakikisha wanazitoa kwa
muda muafaka.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment