Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu
Kadhalika, alisema majangili hao waliingia kwenye mamlaka ya
hifadhi ya Ngorongoro na kuvamia basi la abiria juzi majira ya saa 9:00
alasiri na kuwapora wasafiri fedha na mali.
Nyalandu alitoa kauli hiyo katika mkutano wake na waandishi wa
habari jana jijini Dar es Salaam, kuhusu hali ya ujangili na mkakati wa
serikali katika kupambana nao.
Alisema serikali katika kutekeleza maazimio ya bunge yaliyotokana
na kamati ya James Lembeli, imechukua hatua mahususi ya Rais Dk. Jakaya
Kikwete ya kuunda tume ya kimahakama kwa ajili ya kuchunguza tuhuma
zilizotolewa dhidi ya Operesheni Tokomeza Majangili.
“Tunasikitika sana na taarifa tulizozipata usiku wa kuamkia leo
(jana) majangili watatu akiwemo mwakamke mmoja walimuua faru katika eneo
la Moru, kusini mwa hifadhi ya Serengeti baada ya askari wa wanyama
pori waliokuwa doria kugundua mauaji hayo na pembe zake zilikuwa
zimetolewa,” alisema na kuongeza kuwa.
“Serikali katika kutekeleza maazimio ya Bunge yaliyotolewa na
Kamati ya Lembeli imechukua hatua mahususi na kwamba vyombo vya ulinzi
na usalama vinaendelea na msako wa kuwasaka na kukabiliana na
majangili,” alisema Nyalandu.
Akijibu madai ya dhumuni la mkutano wake na kamati ya ulinzi na
usalama za mikoa ya Dodoma na Manyara, alisema mkutano huo ulihusisha
wakuu wa mikoa, wilaya na vyombo vya usalama kujadili migogoro ya mipaka
baina ya hifadhi ya Tarangire, pori la akiba la Mkungunero na wananchi.
Akifafanua alisema miongoni mwa mambo muhimu yaliyojadiliwa ni
pamoja na Operesheni Tokomeza inayotarajiwa kuanza kwa awamu ya pili.
Alisema serikali imeanza kutekeleza maagizo ya Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira chini ya Lembeli na agizo la rais
la kuundwa Tume ya Kimahakama ili kubaini ukweli wa tuhuma
zilizojitokeza.
“Hali ya ujangili nchini ni mbaya na kwa namna yoyote serikali
itapambana na vitendo hivi vya ujangili na uhujumu uchumi vinavyofanywa
dhidi ya raslimali za Taifa,” alisema.
Akizungumza na NIPASHE Jumamosi kwa njia ya simu, Mkuu wa Mkoa wa
Manyara, Eraston Mbwilo, alisema kwa sasa hali imetulia na kwamba
wananchi wanaondoka kwenye maeneo hayo katika hali ya utulivu.
“Wananchi wanaondoka kwa utulivu na amani imechu
kua nafasi yake, polisi wanaendelea na kuimarisha ulinzi na usalama wa raia,” alisema.
Akizungumzia kuhusu mkutano kati yao na Naibu Waziri Nyalandu,
alisema walijadili kuhusu awamu ya pili ya Operesheni Tokomeza majangili
jinsi itakavyoimarishwa.
“Mheshimiwa Nyalandu alisisitiza ushirikiano katika operesheni
ijayo na alizijulisha kamati za ulinzi za mikoa yetu (Manyara na
Dodoma)… lakini cha ajabu nimesikitishwa na taarifa za uongo zilizozagaa
kwamba Nyalandu alikashifu na kuishambulia kamati ya Lembeli” alisema
na kuongeza kuwa.
“Nashukuru wewe mwandishi, umepiga simu kutaka kujua hali ya
usalama na nini kilitokea kwenye mkutano wetu… tulijadili mambo makuu
matatu, kuanza kwa operesheni awamu ya pili, serikali kutekeleza maagizo
ya kamati ya bunge na agizo la rais kuunda tume ya kimahakama ili
kubaini ukweli wa tuhuma zilizojitokeza” alisema Mkuu wa Mkoa Mbwilo.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment