Home » » WATAKIWA KUWEKEZA MAENEO YENYE MIGODI

WATAKIWA KUWEKEZA MAENEO YENYE MIGODI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Wamiliki wa migodi na wachimbaji wa madini ya Tanzanite, mji wa Mirerani mkoani Manyara, wametakiwa kuwekeza wilayani hapa.
Padri Pastory Kijuu wa Kanisa Katoliki, Parokia ya Bikira Maria alitoa wito huo juzi alipozindua Shule ya Msingi na ya Awali ya Blue Tanzanite.
Padri Kijuu alisema watu wengi wamekuwa wakipata madini hayo na kwenda kuwekeza maeneo mengine, ikiwamo katika miji ya Arusha na Moshi badala ya kunufaisha eneo husika.
“Sio sahihi hata kidogo kuja Mirerani kuchota utajiri na kuondoka nao wote pasipo kuwekeza na kwenda kuwanufaisha Ulaya, Afrika Kusini au kwingine na kusahau sehemu ulipopata mali,” alisema Padri Kijuu.
Alisema mkurugenzi wa Shule ya Blue Tanzanite, Alex Ombade anastahili pongezi kwa kujenga shule yenye walimu, majengo mazuri na eneo kubwa.
Naye Ombade alisema shule yake ilianzishwa mwaka 2008 na hadi sasa ina wanafunzi 360.
“Lengo la kuanzishwa kwa shule hii ni kuhakikisha jamii ya eneo hili inapata elimu bora itayowasaidia katika maisha yao,” alisema Ombade.
Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji wa Mirerani, Albert Siloli alisema Serikali ipo pamoja na taasisi binafsi zinazotoa huduma kwa jamii na itaendelea kuziunga mkono ili kufanikisha maendeleo kwa jamii.
“Tutaendelea kushirikiana na watu kama Ombade ambao wamejitolea kuwekeza kwenye shule kwani watoto wetu wa Mirerani na majirani zetu watapata elimu,” alisema Siloli.
Hata hivyo, mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Magweiga Mack alisema Blue Tanzanite imezinduliwa kwa maombi na sala, hivyo wanasubiri kuweka jiwe la msingi.
 Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa