Home » » IFAHAMU SEKTA YA KILIMO KATIKA MKOA WA MANYARA

IFAHAMU SEKTA YA KILIMO KATIKA MKOA WA MANYARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mkoa wa Manyara una eneo la hekta 1,568,117 zinazofaa kwa kilimo ambapo zaidi ya hekta 867,500 zinatumika kwa kilimo cha mazao ya aina mbalimbali. Eneo la kilimo linabadilika kila msimu kulingana na malengo ya wakulima na mwelekeo wa hali ya hewa.
Pia Mkoa una maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji yanayofikia hekta 30,997 na kati ya hizo hekta 11,715 zinatumika kuzalisha mazao ya aina mbalimbali kama vile mahindi, mpunga, miwa, migomba na mazao ya mbogamboga na matunda. Maeneo makubwa yapo Wilaya ya Babati (Bonde la Kiru) na Simanjiro (Ukanda wa Mto Pangani). Maeneo mengine yapo Mbulu (Bonde la Bashay) na Hanang (Bonde la Endagaw na Gocho)
Mazao yanayolimwa ni Mahindi, Alizeti, Mbaazi, Mtama, Ngano, Maharage, Miwa, Vitunguu Maji, Vitunguu Saumu na Mpunga ambayo hutumika kama mazao ya Biashara na Chakula kwa wakazi wa Mkoa. Ziada ya uzalishaji huuzwa kwenye Mikoa mingine na Nchi jirani za Kenya, Somalia, Ethiopia, Eritrea na Sudani.
Moja ya Mashamba ya Mahindi Wilayani Hanang-Mkoa wa Manyara
Moja ya Mashamba ya Mbaazi Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara
Moja ya Mashamba ya alizeti katika Wilaya ya Kiteto Mkoa wa Manyara
Shamba la Ngano katika Wilaya ya Hanang-Mkoa wa Manyara
Mafanikio yaliyopatikana katika Sekta hii yanatokana na jitihada za Serikali na wadau wa maendeleo katika kuimarisha matumizi ya wanyama kazi, matrekta makubwa na madogo (power Tillers), mbegu bora, mbolea na wataalam wa ugani.
Maksai wakitumika kusafirisha mazao shambani
Mwaka 2006, Serikali ilianzisha Mpango wa kilimo wa ASDP kwa lengo la kuongeza uzalishaji mazao kwa kushirikiana na Mradi wa PADEP “Participatory Agriculture Development and Empowerment Project unaoshirikisha wananchi kuibua Miradi ya Vikundi na Miradi ya Jamii na kuchangia gharama za utekelezaji katika Sekta za Kilimo na Mifugo.
Miundombinu mbalimbali iliweza kujengwa katika maeneo mengi ya Mkoa.
Baadhi ya miundombinu hiyo ni Vituo vya rasilimali za Kilimo na Mifugo, Maghala, majosho, nyumba za maafisa ugani na machinjio.
Aidha, Mkoa unashirikiana na Mashirika na Taasisi za Maendeleo ya kilimo katika kukuza na kuendeleza Sekta ya Kilimo na Mifungo. Mashirika hayo yametajwa katika jedwali lifuatalo na kuonesha majukumu wanayotekeleza.
Chanzo Tovuti ya Mkoa wa Manyara

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa