Home » » CHADEMA WAFANYA MAGEUZI MANYARA

CHADEMA WAFANYA MAGEUZI MANYARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa kimetoa siku 10 kwa uongozi wa chama hicho Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara kufanya uchaguzi ngazi ya chini hadi wilaya ili waweze kupata tiketi ya kushiriki uchaguzi mkuu wa 2015.

Mkuu wa Itikadi na Uenezi Taifa, Waitara Mwita akizungumza na kamati ya utendaji ya chama hicho wilayani Kiteto hivi karibuni alisema, ushiriki wa chama hicho uchaguzi mkuu 2015 utategemea kukamilika kwa uchaguzi ngazi ya chini.

"Hatutaivumilia wilaya yoyote ishiriki uchaguzi mkuu mwakani, kama hawatafanya uchaguzi ndani ya chama na hili tutalisimamia kikamilifu na wala hatutaona haya kulisemea na mahali popote nchini,"alisema

Wakati huo huo, kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA kiongozi huyo ameufuta uongozi wa vijana wilaya baada ya kuonekana wana umri mkubwa na kuchaguliwa Abubakari Kidevu kuwa Mwenyekiti huku Katibu akiwa Athumani Ismail.

Mbali na hatua hiyo pia kura zililazimika kupigwa kuhusu kuvunja kamati ya utendaji ama kutovunjwa kutokana na kuonekana kushindwa kuwajibika ipasavyo ambapo walilazimika kuongezewa wajumbe wengine ili kusukuma mbele shughuli za chama.

"Hali haikuwa shwari kwenye kikao, kwani hata kamati ya utendaji ilitakiwa kuvunjwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kutowajibika ipasavyo hali iliyosababisha kudorora kwa chama kipindi chote,"alisema Ole Loilole Leng'isya Katibu wa Wilaya.

Aidha, Katibu huyo alisema chama kilitakiwa kufanya uchaguzi huo Juni 30, mwaka huu na kwamba kutokana na sababu mbalimbali zilichangia kutofanyika.

Alitaja baadhi ya sababu hizo kuwa ni pamoja na kukosekana kwa amani katika maeneo mengi ya Wilaya ya Kiteto juu ya migogoro ya ardhi ambayo inaendelea hadi sasa na kusababisha madhara yakiwemo mauaji.

Alisema, hali hiyo imekuwa tishio kwa wananchi na hata viongozi wa kisiasa na Serikali kwa ujumla kuendelea kufanya kazi katika mazingira hayo kutokana na kitendo cha mauaji ya kila mara huku kukiwa hakuna jitihada za makusudi kukabiliana na tatizo hilo.

Hata hivyo, CHADEMA kwa pamoja wamelaani mauaji yanayoendelea kujitokeza kwa jamii ya wakulima na wafugaji wilayani humo na kuitaka Serikali kuzuia ili kuwapa wananchi waweze kufanya kazi ya ujenzi wa

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Manyara Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa